Msanii Maarufu wa Bongo Movie, Aunt Ezekiel ameripotiwa kufunga ndoa na Mchumba wake ajulikanaye kama Sunday Dimonte nchini Dubai, Falme za Kiarabu (UAE)
Ndoa hii inaripotiwa kufungwa June 17, wiki 2 tu zilizopita.
Habari zinadai kuwa, Aunt alifikia uamuzi huo baada ya mwanaume huyo 
kumwambia hawezi kuvumilia umbali uliopo kati ya Tanzania na Dubai hali ambayo 
Aunt alihofia kupigwa chini.
Waandishi walimsaka Aunt 
kwa njia ya simu ya kiganjani akiwa Dubai, alipopatikana na kuulizwa kama kweli 
amepigwa pingu za maisha, alifunguka:
“Ni kweli nimefunga ndoa huku Dubai 
lakini nimesikiasikia kuna watu wanasema nilifanya siri. Siyo siri, ila huku ni 
mbali na huko nyumbani Tanzani, isingekuwa rahisi kuita watu wangu wa 
karibu.”
Paparazi: Kwa hiyo ndiyo imetoka hiyo?
Aunt: Hapana, nitakaporudi 
nyumbani nitafanya sherehe, nitaalika watu, hata wewe, tena itabidi unichangie 
jamani.
Ngoja tuone akirudi itakuwaje.Kama ni kweli, Aunt Ezekiel atakuwa amejiunga na wasanii wengine wa Bongo movie waliowahi kufunga ndoa kama Irene Uwoya na Wastara.
Tunaomba iwe hivyo!
HABARI KWA HISANI YA RAFIKI YANGU JOHN KIANDIKA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment