Thursday, May 31, 2012

SINGLE BUTTON EVOLUTION-By Martin Kadinda-PLACE YOUR ORDER NOOOWWW!!

Hii naita ubunifu...Tena wa hali ya juu sana

Martin Kadinda ametumia kile kipaji ambacho Mungu amempa,na amekitendea haki...

FOR YOUR ORDERS CALL 0786 670257...ASK ANYTHING!!


Smart collection kama unavyoona pichani,designed by him...

Huna haja ya kwenda kwa Msambaa kushonesha Suti,imepitwa na wakati

ngalia kazi zake alizokwishafanya so far na watu mbalimbali:

CHEKI HIYO..BOTH MEN AND WOMEN


HAPA NI DIAMOND NA OMMY DIMPLES

MILLARD AYO,B12 WAKIWA WAMETUPIA

DIAMOND,MARTIN,OMMY DIMPLES


WANAWAKE HAMKO NYUMA...VITUUUZZZ

UKIPATA MPENZI FRIED CHICKEN MSHUKURU MUNGU SANA,UKIPATA MPENZI MJUSI WA KUKAANGA KAZA ROHO

Kuna aina ya mtu katika maisha,ukimpata akawa mpenzi wako,unasema asante Mungu, umenipa zawadi hii,he/she is a man and a half,ni kama wewe ni Chips umekutana na Fried Chicken with Mayonnaise,ni raha na kila kitu ni utamu tu na kujilamba..

 Ila kuna mtu unakutana nae, anakuwa mpenzi wako,Kiruu!!Ni kasheshe bin vurugu mechi,Hadi unajikuta unakuwa mtaalamu wa kuimba wimbo wa Shaggy, Why me Lord kila s...iku...Ni kama wewe ni Chips halafu umekutana na Mjusi aliyekaangwa na kachumari ya pilipili,sidhani kama utafeel kula labda uwe Mchina mtengeneza barabara.

 Kama umepata mpenzi wa kweli,sali sana,mshukuru Mungu na umuombee,maana ni bahati sana na vita ya kumkeep ni kubwa,sio unachukulia for granted..
 
.Na pole kwa wewe uliyekumbana na Mjusi,fumba macho mmwagie tomato Ketchup,huwezijua anaweza kuwa na ladha ya prawns

NDOA INAKUPA PETE NA TITLE TU,HAIBADILISHI TABIA YA MTU

Ndoa haibadilishi tabia ya mtu,nyie ambao mna hopes kwamba aah my boy atabadilika tu huko mbeleni tukioana,or my girl atabadilika,habadiliki ng'oo!

 Kama anakupiga ngumi leo be sure atakutandika na mwiko huko ndani...Ukikosea kudhani kwamba Ndoa inakuja na changes utapotea.

Ndoa inakupa pete tu kidoleni na kukuchange title,ila sio tabia.Kama anapenda dagaa leo ndoa haitambadilisha apende matembele.Make the right choices leo lasivyo utakuwa mtumwa wa tabia zake milele.

Kosa kubwa watu hufanya ni kuamini kwa sababu ameamua kuniweka ndani,haya mambo yatakuwa madogo na with time atachange,HAPANA!

Kamwe usithubutu kufanya Assumptions na ndoa,tabia ya mtu kwenye ndoa itaonekana Mapema,huwezi kuona Jua linawaka halafu uwaambie watu sasa hivi ni Sa3 usiku,utakuwa Kichaa.

Ni muhimu kufanya maamuzi sahihi,kwenye muda sahihi,na kwa mtu sahihi,la sivyo,ndoa haitakuwa chaguo sahihi kwako,utajikuta umejifunga kwenye Mateso ya milele!

SIO KILA ANAYEBREAK UP NA WEWE HAKUPENDI

NGUMU KUMEZA:

Sio kila anayebreak up na wewe hakupendi,Ni mkatili,Hajali,Ni player,hana shukrani,au amekutumia kama brashi ya Kiwi halafu anakuacha na dawa nyeusi na kukusokomeza chini ya kitanda

Wengine wanaomba Break Up baada ya kujitathmini na kugundua kwamba wewe,ur too good for them na hawastahili hata kidogo kukumiliki,wanaacha mwenye stahili akupate.Sasa wengine wakiachwa wanaanza shombo,Mwanaume atakuwa Yule,Janaume halina shukrani nimelivumilia tangu liko Kapuku hadi leo linajua hata kuweka panga kwenye suruali!

Kama nimegundua una penzi 100% kwangu na mimi nna 20% kwako nifanyeje?80% yote nakunyonya wewe,nakuwa kama kupe,naamua kuwa mkweli kwa nafsi yangu tu,kwanini nikudanganye na kukupotezea muda nije nikudissapoint baadae wakati nimeshajua mapema,naamua kmuachia mwenye 100/100 aje akupe unachostahili

Je,kuna kosa hapo hadi muanze kubweka kama mbwa koko wa mjumbe kisa umetiwa konzi??

Wednesday, May 30, 2012

NIDANGANYE VIDEO-BRAND NEW-Shetta FT Diamond Platinumz

Jiwe jipya limeingia sokoni,pata uhondo ukiwa bado wa motooooo...Bonyeza LINK hii hapo chini ule Video ya ukweli sana kama kawaida Adam Juma wa Visual Lab ametengeneza Video hatari kabisa.

http://youtu.be/ZZqRcAhar2Q

BIG UP KWAKO SHETTA NA KWAKO DIAMOND KJWA VIDEO HII CLASSIQUE TO BE HONEST

Enjoy!!

Tuesday, May 29, 2012

SOME BROKEN HEARTS NEVER MEND....IKIVUNJIKA YA KIOO TAFUTA KIKOMBE CHA PLASTIKI KWA MUDA

Wakati mwingine Relationship zetu ni kama Glasi ya bei mbaya sana,iliyoanguka kutoka ghorofani,unaipenda sana maana umekuwa ukiitunza kwa uangalifu,na uliinunua kwa gharama..

Lakini...Glasi hii imeanguka na imesagika vipande,kujaribu kuviokota vipande hivi unajikuta unakatwa na vipande vya hiyo glasi,mwili mzima unachuruzika damu kwa Maumivu...

Sometimes,inapaswa tu ukubaliane na matokeao kwamba Glasi hiyo haiwezi kutumika tena zaidi ya kukukata tu...

Tafuta angalau Kikombe cha Plastiki kwa muda,huku ukitafuta Glasi nyingine ya thamani kureplace ile old one...

Some of our Broken hearts will never mend....

KWA WALE WANAUME SELFISH,KUCHEUA DAKIKA 5 MWIKO

Mapenzi ni tofauti sana na Football.Najua wanaume wengi tunapenda Football,inatuharibu sana..Maana kwenye Football watu wanahangaika,mikiki mikiki,vikumbo,rafu ilimradi wapate magoli mengi washinde mechi,wafurahi...



Mapenzi ni tofauti kabisa,makeke yawepo ila sio kwenye kukimbilia golini kucheka na nyavu...Hayahitaji wewe kukimbia wee,kupiga supu ya Pweza na bamia mbichi ili ukako...moe uwanjani...Mwanamke hahitaji maraundi yako kibaooo utadhani mko kwenye Cricket,anahitaji yeye kufunga,concentrate kumuwezesha..wanawake wakiwezeshwa wanaweza,lakini wengi tumekuwa tunajiwezesha wenyewe.

..Tunaharibu!

Kwanza wewe its guaranteed,utafunga tu penati mwisho wa mechi,unakimbilia wapi??Tulia, muwezeshe mama apige danadana,mpe afunge hadi aseme puliza filimbi!kwa vyovyote wewe utafunga la kwako mwishoni tu,sasa kimuhemuhe cha nini kucheua uji wa ulezi kwa dakika 5?

Monday, May 28, 2012

NSA-No Stress Allowed Season 3 @ Bagamoyo...

Tumeamua kuambukiza watu upako wa kuwa na furaha muda wote...

Haturuhusu mtu yeyote kukosa furaha,at any time...we have created this event,makusudi kupambana na adui anaitwa STRESS....as long as Mungu amekupa uhai na unaishi,unatakiwa kuwa na furaha na Raha muda wote, and this is it...

Weekend hii ya tarehe 26 na 27,tukajibeba hadi Pwani ya Ufukwe wa bahari ya Hindi,pande za Bagamoyo..tukasahau shida zote...Tukaongea...Tukabwaga Mioyo yetu...Tukajifunza mengi sana kwa masaa mengi sana...Tukafurahi....Na tukarejea tukiwa watu wapya....na Furaha tele.

GET READY,tukio linalofuata litatukia tarehe 28 na 29 July, usiplan kukosa kabisaaaaaaaaa

Baada ya Camp 2 za mafanikio na shangwe kwenye Pori na Uwanda tulivu wa Pugu Hills, The Pugu Hills Magic,safari hii Bagamoyo ilitutendea haki sanaaaaaa...

Picha za Shangwe na Matukio ndo hizi hapa chini.....


CHADEMA TULIKUWEPO



DAVIE,OUR ESTEEMED GUEST ALL THE WAY FROM ATLANTA, GEORGIA FOR THE CAMP...OOH YEAH


MIMI NA MOUNTAIN DEW,MNISAHAU TU

DAVID NDAIGA WEAR ILIWAKILISHWA VEMA NA DORICIOUS CINYORITA

TUKAPAMBANA KIDUKU

SHOW LOVE,JOSEPH,EVE,AND KATAZA

DAVIE,BABY,TINA,SAJO AND JP

6 USIKU TUNAGONGA VYUKU TU HATUNA HABARI

THATS THE POOL VIEW

HAPA NDO TUMEFIKA SWIMMING,TUKALA POSE HAPO,MI NIKALALA KABISAAAAAA


COOKING TIME,WIFE MATERIAL WAKIWA KAZINI,TINA,TUSEKILE,ATUPULIKE AND EVELINE...MKO VIZURI SANA GIRLS

MPANGO MZIMA...CHEKI SWIMMING HIYOO

SAA 9 USIKU HIYO,NI PICHA TUU

 ZEE LA KICHAGA,EVE,NA ABRAHAM







CHIEF POLITE KAMETTA AKIWAZA ATAKAVYOZAMA KWENYE SWIMMING POOL

ATU,ME,KATAZA,KULA GUDI TAIMUU

CHEZA OLIVA TWIST HAPOOO

MISOSI YA ASUBUHI KABLA YA SWIMMING


 JAMANI MNANIONEA MZIGO WOTE HUU..NI KAMA NILKUWA NALALAMIKA FLANI HIVI
 HUSBAND MATERIALS....POLITE,SETH,JP,AND DAVIE
 HAPPY HAPPY MOMENTS EVER SEEN
 MUDA WA KUBWAGA MOYO UKAFIKA...NO STRESS ALLOWED
 HUSBAND MATERIAL JP AKISAIDIA KUBEBA MIZIGO,SALUTE KWAKO MKUU
MAMA USHAURI,EVELINE
 MISOSI KIBWENAAAAA KWA AFYA
 MJUKUU WA KINGWENDU SA 10 USIKU,HAHAHAHA JP ULITISHA SANA
 CHIEF COOK WETU AKIPIKA VYUKU WA UKWEE
 SEE FOR URSELF,BAHARI INAPULIZA SAA8 USIKU,MNATAFUNA TUUU
 MAMA LAO,EVE
 NIKAWAONYESHA ILE SHAMUKWALE INAVYOPIGWA
 JP AKAJARIBU KUSHINDANA,MCHAGA NA KUCHEZA WAPI NA WAPIII
 KIDUKU BIN KIBEGA,YEBAAAAHH
 ENGINEER WA PWP CAMP AKIGONGA VYUKU
 DORICIOUS,JP NA LUSAJO WAKIPOSE
 ANHAAAA,ONGEZA KUKU HAPAAAAA

 SALOON IKAFUNGULIWA UFUKWENI

 MAMAA TUSEKILE AKITUPIGA STORI NYOKA
 JP ULIAMKA VIZURI SANA WEEKEND HII,FULL VITUKO
 POLITE NA ATU WAKIFUKUZA USINGIZI 11 ALFAJIRI,CHEZEA KIPUPWE

 THE MAN FROM ATLANTA ANASINZIA,10 USIKU,INATAKA MOYO,BABY NAJMA PEMBENI
 MADIKODIKO MANJALI MAPOKOPOKO
WAO WANAKULA MI BADO NASWING TU

GONGA SANA VYUKU AISEE


TINNA NA JP,KUKU TYME

HAPANA CHEZEA BARIDI LA SAA 10,MASHUKA NA VIKOI MUHIMU

MAMAA TUSEKILE MWAKYEMBE,MAWAZO YA FUNGUO HAPO!

MZEE WA VIANDE...LUSAJO

WE JP UNAMDANGANYA NANI SA 9 USIKU

BABA PAROKO POLITE
 CNYORITA DORICIOUS
 WAKUU WA KAYA,ME AND KATAZA TUKIMSIKILIZA MTOA MADA
 KATAZA NA EVE WAKIWA MAKINI KUSIKILIZA HOJA