Wednesday, June 27, 2012

HIVI NDIVYO DK ULIMBOKA ALIVYOTEKWA-KAMANDA KOVA

Akizungumza na waandishi wa Habari Mchana huu, Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, amesema Dk Ulimboka alitekwa na watu wasiojulikana akiwa Leaders Club akinywa pombe, pale Kinondoni


Kamanda Kova amesema Ulimboka aliokotwa na msamaria mwema ambaye hakutaka kumtaja jina lake kiusalama na kutoharibu upelelezo kuwa msamaria mwema huyo.


Dokta Ulimboka aliokotwa katika msitu wa Mabwepande na msamaria mwema aliweza  kutoa taarifa kituo cha polisi cha Bunju, ambapo polisi aliyekuwa zamu alichukua maelezo yake na baadae Steven Ulimboka kuletwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.
Kamanda Kova amesema jeshi la Polisi Kanda Maalum limeunda jopo maalum kwa ajili ya uchunguzi na upelelezi wa tukio hilo la utekaji nyara, kwani ni tukio la kwanza kutoke nchini, ameongeza kwamba wahusika wote watakaobainika kuhusika na tukio hilo wachukuliwa hatua za kisheria na sheria itafuata mkondo wake ili kukomesha matukio mengine kama hayo

WAANDISHI WA HABARI WAKIMSIKILIZA KAMANDA KOVA


KAMANDA KOVA AKIONGEA NA WAANDISHI MCHANA HUU


Hii ndio hali ya dokta Ulimboka alipofikishwa Muhimbili Hospital.Inatisha aisee kama Tanzania tumefikia hali hii,amani iko wapi!




HAPA AKIWA NA WAZIRI MKUU PINDA..NA MIKONO WAKASHIKANA



Dokta Ulimboka akionekana pichani wakati wakiwa kwenye mgomo wao wa mara ya kwanza na madaktari wenzake

No comments:

Post a Comment