Friday, June 8, 2012

HOW TO WIN MOYO WA MWANAUME...ITS SIMPLE

Kibiblia Mwanaume ni kiumbe anayeaminika kuwa kichwa wa Familia...Lakini practically Mwanamke anarun  show ya Familia,hilo liko wazi labda ulete tu ubishi wa Kimasai kwenda kwenye harusi na Suti ya Lubega....

Mungu aliona Mwanaume anahitaji usaidizi,akamuumba Mwanamke aje kumsaidia...Roile ya Mwanamke ni kumsaidia pale ambapo Mwanaume hakukamilika akiwa mwenyewe..

TWENDE SAWA!

Wakati ambapo Wanawake ni viumbe very complicated,na sio tu complicated kwa sababu tunapenda kuwaita hivyo lakini hata Uumbaji wao ulikuwa complicated...

Mungu ilibidi amlaze Adam usingizi....

Ili achomoe ubavu,kumuumba Hawa...

Kwanini amlaze usingizi???Adamu angekaa macho,asingeamini process ya kumuumba msaidizi wake! Sidhani kama angevumilia,angekata tamaa jinsi ya kuhandle uumbaji mgumu namna ile,Mungu akampa dozi,akasinzia...Yaliyojiri wakati akiwa usingizini ni makubwa sana,na ndio maana kuishi na Mwanamke inapaswa utumie akili,na hata Biblia imesema,Enyi Wanaume,ishini na Wake zenu kwa akili,Mungu anajua,they are complex...

Wanaume ni viumbe very simple...Kuna watu huenda mbali na kusema,Kwa Mwanaume,Jibu la Yes na No,vyote vina maana Moja...Maana yake ni kwamba Wanaume ni watu simple,wasiojali sana mambo! Wanawake wanajali details...Na ndio maana ni wasaidizi,pale ambapo Mwanaume anaona kila kitu ize ize,Mwanamke anasema hapana,sio ize kama unavyodhani,anajazia kinachopaswa...

Sasa basi,baada ya kuelewa jinsi gani nature ya Mwanaume na Mwanamke zinapopishana,Mwanamke hatakiwi kucomplicate jinsi ya kuishi na Mwanaume...Kanuni za Mwanaume ziko wazi na zinaeleweka..

Mwanaume hahitaji mambo makuuubwaaaa ili ajue anapendwa,very small,tiny things,vinakaa sana moyoni,na kwa muda mrefu...Wala Wanawake msitumie muda kufanya mambo makubwa kutafuta kumu-Impress,WALA!

Mwanaume anaweza kuwa impressed na jinsi unavyompikia...Jinsi unavyomfunga tai..jinsi unavyobrush viatu...jinsi unavyopiga pasi...Jinsi unavyosafisha nyumba,na SIO jinsi unavyomkaripia akikosea,jinsi unavyoshika simu yake mara kwa mara kumpekua,unavyomfuatilia yuko wapi,na nani na kwa nini,tena kwa maswali ya kuudhi.Wanaume hawapendi,hizi ni Complications za kike na kwao THEY DO NOT WORK!

Ukitaka umkose Mwanaume,basi fanya vitu vya KIKE,ukitegemea utamcontrol,matokeo yake ni dhahiri,utampoteza.

Ni rahisi sana Mwanaume kufanya SWITCH,kutoka kwako,kwenda kwa mtu mwingine anayefanya vitu SIMPLE kwake,na ukashangaa why ameenda kule wakati wewe umekazana na big stuffs,He doesnt look for BIG stuffs to be impressed!

GIRLS,Men are simple,and you should keep it simple....Kumgombeza ni DONT kwake,Kununa ni DONT kwake...Kumkagua ni DONT....Kumuuliza maswali kuhusu uhuru wake,na hii ndo mbaya kabisa ni DONT maana Wanaume wanapenda uhuru wao kuliko chochote...Kama ni necessary kuhoji uhuru,kuwa mwangalifu jinsi unavyouliza,dont go direct,find a way to ask for uhuru kidogo from him na umuache afeel guilty kuamua baada ya kuwa umepeleka request na sio KUORDER afanye...

Kwa leo inatosha....Remember,SIMPLE....thats the rule for MEN!

3 comments:

  1. Well said father blog, tujifunze wanawake jamani....wengine wanaangaikaga kwenda hadi kwa waganga kumbe walaaaaa, ni kujua tu jinsi ya kumu handle mwanaume

    ReplyDelete
  2. wengine ukiwaacha huru wanakufanya ww poyoyo.. watalala huko huko, watapokea simu za vimada mbele yako ,na ukimchekea chekea next time anakujia na kimwana live na uendelee kutabasamu tuu.lol

    ReplyDelete