Friday, May 11, 2012

MAUMIVU YA MAPENZI HAYATIBIWI NA HEDEX



Maumivu ya Kichwa huanza taraaaatiiibuuuuu...Meza HEDEX

Maumivu ya Mapenzi huanza taraaaatiiibuuuuuuuu,mnanuniana siku 2,mnarejea..mnatukanana..mnanuniana wiki..mnarejea...mnapigana mnanuniana mwezi hadi marafiki wanapatanisha..mwishowe chaliii....Mapenzi hayana HEDEX useme utameza,maumivu yake ni aidha uyasikilizie hadi bichwa lipasuke au utafute njia kuyakimbia hayo maumivu..
Poleni sana mnaoumw...a mapenzi,Unampigia mpenzi wako sa6 usiku simu iko bize wakati aliaga analala sa 4,ukimuuliza kesho yake anasema ni network tu baby na we ulivyo boya unaamini..pole sana wewe usiyejibiwa message anasema yuko bize ila ukibadili simu ukitumia ya rafiki yako anajibu fasta ndani ya sekunde 30...Pole wewe unayepigwa na huyo mwanaume kisa mapenzi,una michubuko kama Jambazi kila kona ya mwili lakini bado unasema in a relationship with...Poleni mlioolewa lakini mmegundua ndoa sio mchezo kama FUTUHI mnatamani kutoka...Poleni sana..Kungekuwa na HEDEX ningewauzia ila kwa sababu hamna we umwa kichwa tu...

No comments:

Post a Comment