Saturday, September 15, 2012

NINI KIMEFANYA WANAUME KUTOKUWA NA HURUMA NA WANAWAKE THESE DAYS

Iam back....Sorry kwa kuwa kimya kwa muda,hii ni kutokana na kubanwa na mmbo ya hapa na pale katika kujenga nchi...

Leo tujadili hili...Na sababu kubwa iliyonifanya nilete mada hii ni kutokana na mambo ninayoyaona,watu wengi wanazidi kulalamika,na baadhi ya watu wa karibu wamekuwa wakinieleza jinsi wanavyoumizwa...Na hawa wengi ni wadada

Wadada wengi siku hizi wanalalamika wanaume wamekuwa Mbwa...Na ninakubaliana nao kwa asilimia 100..Kweli Wanaume wamekuwa Mbwa haswa....Hawajali anymore...Lakini nini kimesababisha Wanaume kuwa Mbwa siku hizi...Twende pamoja

1.GENETIC REASON

Kwa jinsi wanaume walivyoumbwa,wameumbwa wawe watu wa control...Na hii ni Kibiblia kabisaaa..Na hata socially iko hivyo

Kutokana na hii sababu,ikitokea Mwanaume akakupenda kiukweli kutoka moyoni,ambayo ni nadra sana kutokea,anatamani awe na control,ambayo ni nature...Control over you in terms of Ownership...Akumiliki peke yake...Na kama amekupenda,akatamani akumiliki,halafu wewe ukashare milki yake,kitu kitakachotokea hapo ni hasira ya Usaliti uliotukuka sana ambao huwa hauponi kirahisi..Si kwa kupenda ila ni nature...Naturally,Mwanaume kugeuzwa fala ni Abomination kubwa sana..Hata ikitokea miaka 20 iliyopita,haiponi haraka.Msiwalaumu wanaume,haiponi haraka na kila siku,na kila saa ataingia in Love with the notion of what happened,hataamini tena katika kumpa Mwanamke moyo wake...Na hapo ndipo shida inapoanzia,hatajali...Ukiumia au Usiumie kwake yeye ni sawa coz Moyo wake hauko 100% invested so hes in his comfort zone.

2. HISTORICAL REASONS

Wanaume kihistoria huwa wanakuwa na mahusiano mengi kuliko wanawake..Wanawake huwa wana sense of shame kwenye idadi ya wanaume wanaolala nao(with exception to bitches who dont care)...So kwa Mwanaume kuwa na listi ya wanawake 15 ni kawaida,wakati Mwanamke akifikisha 6 nafsi inamsuta kwamba sasa anajaza kontena...

Hii imewafanya wanaume kuwa exposed na mambo mengi sana kuhusu Mapenzi kuliko wanawake....In 5 years,Mwanaume anaweza kuwa na mahusiano na Wanawake hata 10...KAtika hawa 10,kila mmoja alikuja na rangi yake...Huyu anamtenda kwa style hii...Huyu style ile...So in 10 girls,anakuwa amewajua Wanawake vizuri na all types...Akija kwako wewe Mwanamke wala anakuwa sio mgeni,ukifanya jambo anarecall nyuma kwamba kilipotokea hicho Something happened...Na kwa Mwanaume kama alitendwa kwa style hiyo 5 years back na mtu,halafu wewe unakuja kumfanyia remix leo,usitegemee huyo atakuwa na huruma na wewe...NEVER! Atajua whats next na hatojali kukupush hadi wewe unapotaka kufika,hata kwa fork-lift

In general,Mwanaume aliyeumizwa kamwe hatajali kwa sababu ataona wanawake wote ni sawa,which is not true,lakini Wanawake,epecially wa siku hizi mmekuwa Chronic,hamtabiriki kama Mvua za Dar,muda wowote zinanyesha bila Mamlaka ya Hali ya hewa kutrace your occurence,so wanaume wamejitune..Anytime wako Standby kama FFU na Maandamano ya Chadema,na hapa ndipo Wanawake wengi wanapoumizwa.Wengine ni wema tu lakini mmekumbana na Wanaume waliopokea visago ambavyo kupona kwake ni kwa neema ya Mungu,usipoweza kumtibu vizuri basi utaumia tu,na wengi wenu hamna muda wa kuwajua boyfriends zenu,mko bize kuomba hela za Mawigi tu....

3.MAMBO WANAYOYAONA

Wanaume wanashuhudia vituko kila kukicha kwa marafiki,na ndugu zao wa kiume wanavyofanyiwa na wanajiuliza maswali mengi sana...Wameona rafiki zao wa karibu walivyotendwa baada ya kutendwa na jinsi inavyopain,na wengine hata wamejiua au wamekuta wakiua bila kukusudia kwa uchungu uliowapata.

Hii inatoa alarm na Warning kwao kwamba kuwapenda Wanawake ni kitu hatari sana...Haya yanatokea kila siku na kila leo

USHAURI KWA WANAWAKE

Unapoingia in love,kama umeingia nae inlove for future,find time kumjua huyo Mwanaume yukoje...Ametoka wapi...nini kilimsibu...Na Je,utawezaje kumsaidia kuiondoa negative notion..Usiassume Mwanaume uliyempata ni bikira kwamba atafall in Love....Watu wamegongwa sana huko nyuma,wanaumwa Love Concussion...Ukimchukua tu uakanza nae mahaba na mizinga juu hutajua wapi moyo wake uliumizwa,ur future dreams will die,I guarantee you...Find time umjue Mwanaume wako,Wanaume wengi wameumizwa huko nyuma na vidonda vya Wanaume haviponi kirahisi kama vyenu...Wanawake ni rahisi kusahau vitu,Wanaume sio..inawezachukua zaidi ya Miaka 10 kupona na mpaka apate daktari sahihi.Je, Wewe ni mwanamke daktari sahihi kumtibu ili ujenge family??Kama sio my dear ur finished.

USHAURI KWA WANAUME

Sio kweli kwamba Wanawake wote ni sawa,ingawa percentage wise,wengi wanafanana...Nao wametendwa pia so siku hizi nao wamekaa standby...Find muda kumjua Mwanamke wako ni wa aina gani...Msaidie kama nae ana matatizo,if she is a visionary girl tafuteni where ur interests lie,mjenge familia...Sio vema kumjudge Mwanamke kwamba she is all the same kama wengine,wengine mioyo yao ni Mitakatifu kuliko Papa wa Vatican...

ASANTENI!

No comments:

Post a Comment