Sunday, June 3, 2012

JIFUNZE KUTAFUTA SPANA SAHIHI KWA NATI YAKO..KINYUMECHE CHA MTEMA KUNI UTAKIPATA

Ukiona watu wanasemwa kwamba WANAENDANA....Wanaonekana they look alike,they think alike..they live happily kwa sababu hiyo,haimaanishi watu hawa wanafanana...

Kama jinsi ilivyo nati namba 17...Ina tundu lenye Radius sawa na Spana namba 17....Kwahiyo Spana namba 16 au Spana namba 18,haiwezi kufanya kazi ya kufungua nati namba 17...

Chemisty/Kuendana maana yake ni kwamba lile tundu limekutana na Nati ianyofit tundu

Si kwamba watu wanaoendana wamefanana tabia,HAPANA....Strengths alizonazo Mwanaume ndizo Weakness alizonazo Mwanamke,na hali kadhalika Weakness za Mwanaume ndizo Strength za Mwanamke...watu hawa siku zote huwa wana-arrive kwenye hesabu sawa na Balanced..

Pale ambapo Mwanamke huyu yuko Weak,yule Mwanaume anakuwa na Uwezo wa kumsaidia huyu,so they win..

Pale Mwanaume huyu yuko Weak,yule Mwanamke anakuwa na expertise kwenye hilo eneo,na wanawin.

Utashangaa wanawin vipi...Mwanamke ni mkorofi,jamaa ni Mpole sana...Unaweza kudhani Mwanamke anamuoea yule jamaa lakini walaaaaa,nati imekumbana na Spana Sahihi...Laiti angepata Mkorofi basi ingekuwa Spana namba 18 na isingefit.

These are the secrets...Jifunze kutafuta Spana sahihi kwa Nati yako..Ukipotea hapa,cha Mtema Kuni utakipata!

1 comment: