Tuesday, July 3, 2012

UKITAKA KUUA PENZI LAKO FANYA HAYA HAPA,FASTA TU

Ukitaka kufa mwakani unatakiwa kufanya mambo flani ya hovyo hovyo mwaka huu,utakufa tu..

Ukimeza dawa ya sumu usitegemee itageuka kuwa ARV,itakuua tu

Kuna aina flani ya watu wanapenda sana kujitafutia matatizo,wakiwa In love huwa wanajaribu kuwa too much,kwa vitu ambavyo sio vya msingi hata na havimuongezei lolote zaidi ya matatizo.

Kuna vitu ukifanya unajua kabisa kwamba vitakusaidia kupalilia penzi lako,kuliwekea mbolea ili likue zaidi...Concentrate kufanya hivyo

Ila kuna watu huwa wana-opt kufanya mambo ambayo yanawaua wao wenyewe na mwisho wa siku huishia kujuta tu.

Baadhi ya Mambo ambayo yameua mahusiano mengi sana na yanaendela kuua hata leo,na hata kesho yataua ni haya yafuatayo,Chonde chonde usifanye haya maana huwezi jua Damage ambayo yanafanya kwenye uhusiano wako:

1.MISTRUST

Sifa moja ya Penzi imara ni lile ambalo mnaaminiana...Mtu anaweza kuaga kwenda home na ukajua anaenda home kweli bila kuwa na chembe ya shaka kwamba atachepuka na kufanya Call Diversion.Ukiona penzi ambalo halina Trust,hilo penzi liko ICU na litakata Roho muda wowote.Hamtafika popote. Mistrust huwa haiji hivihivi,huwa ni zao la mambo mengi yaliyotokea ambayo yamemfanya mmoja kati ya wapenzi kupunguza imani na mwingine.Dawa ni kuhakikisha mnamaintain highest level of Trust at all time.Na moja ya njia rahisi sana ya kurudisha trust iliyopotea ni kuwa wawazi...Wawazi kwenye ratiba zenu za kila siku..Thats through Communication..Hakikisheni mna communication  muda wote,ifanyeni kuwa ratiba na sio utumwa,itawasaidia kuwa in touch na kila mmoja atajua ratiba ya mwenzie na kuwa at peace

2.EPUKA U-SPY

Kwenye Mapenzi hakutakiwi kuwa na mtu yeyote aliyesomea CCP Moshi...Hiki ni chuo cha mapolisi na maspy wa usalama wa taifa....Mapenzi ni eneo huru ambalo kila mmoja anapaswa kuwa huru....Sio mpenzi kaacha simu tayari umekwapua...Kuna vitu haviko kwenye Katiba ya Muungano...Simu ya Mtu ni personal property yake..Dont sneek,dont Spy...Ukimuomba simu kuitumia kupiga au kutext usijifanye spy na kuchungulia Inbox..Akigundua atakumind na itakuwa big issue...uhuru wa mtu binafsi uheshimiwe,haikusaidii lolote sanasana utakumbana na vitu ambavyo hutapenda utaishia kununa na kumbe hujavielewa..We are so different,mahusiano yangu na watu wangu niliozoeana nao ni tofauti na wewe...U can see messages na ukadhani ni za cheating kumbe ni kawaida...Stay safe...Dont be a police...Dont Spy,hata uwe tempted namna gani..hii imewacost wengi sana,BEWARE

3.EPUKA UBIZE

Ubize ni msala.Ukikubali kuwa mpenzi wa mtu jua kuna uhuru unapoteza...Japo uhuru kidogo...Mpenzi wako anakuwa priority na ni jukumu lako kuhakikisha anapata Attention....

Ndio unasoma lakini una mpenzi,dont replace him/her with books

Ndio unafanya kazi,una vikao,na assignments,na presentations,na warsha,na kila kitu ILA,una Mpenzi...Dont replace him/her with ur job...Kama huwezi kumanage Shule na Mpenzi....Kazi na Mpenzi....Chonde nakusihi,BE SINGLE,lasivyo utazingua tu mtu wa watu,atafeel hapendwi...hajaliwi..Atacheat,...na wala usimlaumu maana wakati ukiwa bize na mshule wako na mkazi wako,kuna mtu alikuwa na kazi na alimjali...Swali kwake ni Je,kwann huyu ameweza and my Boy ameshindwa???USIMLAUMU LIKITOKEA HILO,kosa ni lako 100%

4.EPUKA EXPECTATIONS

Kuna watu hawana simile...Dakika 2 tu nyingi wamewaza Mbinguni...

Mapenzi yanataka Patience....Anzeni mapenzi vizuri...Know him/her.....Jadili mustakabali wenu pamoja,akupe views zake....Then kama kuna kitu cha kuwasongesha mbele kila mmoja aseme/....Kama kuna vikwazo vya kusonga mbele kwenye hatua kubwa zaidi kama Ndoa mathalani,viwekwe wazi

Ni jambo liko wazi,kuna watu ni wazuri kuwa wapenzi tu lakini sio waume....Kuna watu wanafit kuwa Girlfriends tu lakini sio Wife material....Thats the naked truth

Mtu huyu ukimforce awe mume au mke inakula kwako....

Ndoa ni Institution maalum kwa watu maalum kwa sababu maalum

Kama wewe sio Mtu Maalum usiingie kwenye hiyo Institution Maalum maana hutakuwa na sababu maalum

The point is,usiexpect makubwa katika muda mfupi...give yourselves time to see ile sababu maalum ya kuwaingiza kwenye jukumu maalum..mkiona maono yenu hayaoani kufika kule usiforce...
Hakuna sababu ya kuwa fancy wa Ndoa halafu mkae Mwaka 1 muachane,utakuwa umejichafulia CV bure wakati ungeweza kutulia ukapata the right guy or right woman

Dont be over-ambitious....Stay in ur lane and choose the best out of the rest

2 comments:

  1. yote uliyosema ni kweli mtu wangu.utafikiri umepitia colege ya haya mambo.mimi binafsi nimepitia yote hayo.na nimejifunza sana.ni kweli mtu akiweza kutekeleza uliyoyasema ataenjoy sana.big up sana.nawashauri wayachukue nakuyafanyia kazi alafu wataona utamu wake.hakuna penzi tamu kama penzi lenye hayo mambo uliyoyasema.ni tamu mno.

    ReplyDelete
  2. Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.

    Mume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
    Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
    Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.

    Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
    Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
    Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
    Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
    Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
    Nitaendelea kushukuru milele.
    Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
    . Usaidizi wa kurejesha ndoa
    . Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
    . Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
    . Mwongozo na ulinzi wa kiroho
    Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159

    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete